Mafunzo
Vipaumbele katika Mafunzo ya Kituo cha Urithi wa Ukombozi wa Afrika
-
Kujenga Uwezo wa Wataalamu: Kuendesha mafunzo endelevu kwa wataalamu wa urithi, makavazi na nyaraka kuhusu mbinu bora za uhifadhi na usimamizi wa urithi.
-
Elimu ya Historia ya Ukombozi wa Afrika: Kutoa mafunzo yanayoongeza uelewa wa historia, falsafa na mchango wa harakati za ukombozi wa Afrika.
-
Uhifadhi na Uwekaji wa Kumbukumbu Kidijitali: Kukuza ujuzi wa matumizi ya teknolojia katika uhifadhi, uorodheshaji na usimamizi wa kumbukumbu za urithi.
-
Utafiti na Ubunifu: Kuimarisha uwezo wa kufanya tafiti na kuandaa machapisho yanayohusu urithi wa ukombozi wa Afrika.
-
Elimu kwa Umma na Vijana: Kuandaa programu za mafunzo na uelimishaji zinazokuza uzalendo, utambulisho wa Kiafrika na utunzaji wa urithi.
-
Ushirikiano na Kubadilishana Uzoefu: Kukuza mafunzo ya pamoja na taasisi za urithi, makavazi, vyuo vikuu na wadau wa ndani na kimataifa ili kubadilishana maarifa na uzoefu.