Malengo
Lengo Kuu
Kutambua, kulinda, kuhifadhi, kuendeleza na kutangaza Urithi wa Ukombozi wa Afrika kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Malengo Mahsusi
Kituo kinalenga kutekeleza malengo mahsusi yafuatayo:
i. Kufanya tafiti, kuandaa nyaraka na kuweka kumbukumbu na kutangaza urithi wa ukombozi wa Afrika;
ii. Kutambua na kuenzi mashujaa wa harakati za ukombozi wa Afrika;
iii. Kujenga uwezo wa kitaalamu wa watendaji na wadau katika kutambua, kulinda, kuhifadhi, kuendeleza na kutangaza Urithi wa Ukombozi wa Afrika;
iv. Kuimarisha ushirikiano na uratibu miongoni mwa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika na wadau wengine katika usimamizi, uhifadhi na uendelezaji wa Urithi wa Ukombozi wa Afrika;