Iliyokuwa ikijulikana kama kambi ya FRELIMO eneo la Airport, sasa ni shule ya sekondari ya Samora Machel ipo:-
Kijiji cha Iyera
Kata ya Iyera
Tarafa ya Iyunga
Halmashauri ya Jiji la Mbeya
Katika Mitaa ya Jiji
Katika baadhi ya mitaa ya jiji la Mbeya wapigania uhuru walikuwa na makazi yao kama ifuatayo:-
Wana-Msumbiji walikaa mtaa wa “Game” – eneo la Ghana.
Wana-Zimbabwe walikaa mtaa wa Marwa – eneo la Ghana.
Wana-Angola walikaa mtaa wa “Circle” – eneo la Uhindini.
Waliochanganyika walipanga eneo la Soko Matola zilipokuwepo nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na sasa zimebomolewa.
Nyumba walizokaa katika mitaa ya Game, Marwa na Circle ni mali ya watu binafsi.